Jump to content

Ubao wa matangazo wa Bodi ya Shirika la Wikimedia Foundation/Mitindo ya kimataifa na Uimarishaji wa mtazamo wa Wikipedia wa kutoegemea upande wowote

From Meta, a Wikimedia project coordination wiki
Ujumbe huu, "Mitindo ya kimataifa na uimarishaji wa mtazamo wa Wikipedia wa kutoegemea upande wowote", ulitumwa na Natalia Tymkiv tarehe 27 Machi 2025.

Mitindo ya kimataifa na kuimarisha mtazamo wa Wikipedia wa kutoegemea upande wowote

Wapendwa,

Maryana na mimi tulitaka kuwahabarisheni kwenye chapisho hili la Diff kutoka kwenye Shirika la Wikimedia Foundation[1]. Inaonesha kazi ambayo imefanywa - kuanzia 2022 - kutambua mwelekeo wa kimataifa ambao Shirika na harakati zetu kwa ujumla zinahitaji kushughulikia katika kuuliza ni nini ulimwengu unahitaji zaidi kutoka kwetu sasa.

Ili kuunga mkono jumuiya za Wikimedia na kuthibitisha dhamira yetu ya kutoegemea upande wowote, Shirika la Wikimedia Foundation litakusanya kikundi kazi cha wahariri, Wadhamini, watafiti na washauri wanaofanya kazi ili kuchunguza mapendekezo ya viwango vya pamoja vya sera kuhusu mtazamo wa kutoegemea upande wowote (NPOV) kwa miradi ya Wikimedia inayoweza kulinda Wikipedia, kuongeza uadilifu wa miradi yote inayofadhiliwa na wasimamizi zaidi, na kuamini zaidi sera hizi.

Kuna maelezo zaidi hapa chini na njia za jinsi ya kuchangia. Unaweza pia kupata taarifa hii kwenye Meta.

Mitindo ya kimataifa

Mwaka huu, mojawapo ya mitindo ya kimataifa ambayo imezua mazungumzo muhimu ndani na nje ya harakati za Wikimedia inahusiana na kutoegemea upande wowote: jinsi imani katika taarifa mtandaoni inavyopungua na mgawanyiko wa makubaliano kuhusu taarifa gani ni za kweli. Wengine wanaamini kwamba ulimwengu umekuwa mgumu zaidi, na watu wamegawanyika zaidi kuliko hapo awali. Kwa vile vitisho vya kutoegemea upande wowote vinaonekana kuongezeka duniani kote, sera ya NPOV inahitajika sasa kuliko wakati mwingine wowote. Kanuni hii ya msingi imeitumikia Wikipedia vizuri sana, na imekuwa na nguvu zaidi kwa karibu robo karne ya michango ya watu wa kujitolea.

Jinsi kanuni hii ya kutoegemea upande wowote inavyotafsiriwa katika sera ya NPOV inatofautiana katika miradi ya Wikimedia, ikiangazia fursa kwa jumuiya kujifunza kutoka kwa kila mmoja; na kuchunguza kama viwango vya kawaida vya kimataifa vya kutoegemea upande wowote vinaweza kulinda miradi vizuri zaidi (na watu wanaojitolea) katika mazingira ya vitisho vilivyoongezeka na udhibiti unaoongezeka.

Kama ilivyo kwa sera zote, NPOV imeboreshwa kwa zaidi ya miaka 24 na maelfu ya maoni katika mamia ya lugha. Katika mchakato huu wa mageuzi wa majadiliano ya jumuiya, kanuni ya mtazamo usioegemea upande wowote na matumizi yake yanasalia kuwa msingi kwa mtindo wetu.

Sera za NPOV

Mapitio ya haraka ya sera za NPOV katika matoleo mbalimbali ya lugha ya Wikipedia katika warsha ya hivi majuzi ya jumuiya ilionesha mabadiliko, kutofautiana, na fursa nyingi za miradi tofauti ya Wikimedia kujifunza kutoka kwa kila mmoja. Watumiaji wenye haki za nyongeza, wale wanaoaminiwa na jumuiya zao katika kusimamia sera za NPOV, walielezea changamoto wanazokabiliana nazo wakati sera hizi zikiwa haziko wazi au hazijaendelezwa katika baadhi ya lugha au miradi.

Kadiri imani ya umma katika vyanzo vya habari inavyozidi kupungua[2], wahariri wanakabiliwa na changamoto zinazobadilikabadilika katika kuwakilisha maoni kutoka kwenye vyanzo vya kuaminika kwa haki, sawia, na bila upendeleo wa wahariri. Kama unavyojua vyema, uadilifu wa Wikipedia - hasa juu ya mada zinazobadilika na zinazogombana - unalindwa na michakato thabiti ya utawala wa jumuiya, kwa mfano, sera kuhusu suluhisho la mizozo kwenye Wikipedia ya Kiingereza (k.m., itifaki za majadiliano, mbinu za uangalizi, njia za utatuzi wa migogoro) zinazotanguliza mbinu ya haki na usawa. Viwango hivi vilivyothibitishwa vyema vimeundwa mahususi ili kuzuia ushawishi usiofaa na kuhifadhi muundo unaojitegemea, usio wa faida ambao haupo popote katika kiwango hiki. Tumeona mara kwa mara kwamba watu wanaojitolea wana rekodi nzuri ya kusimamia kwa mafanikio kutoegemea upande wowote kwenye mada zinazozozana.

Sera kali za udhibiti wa maudhui zinazoongozwa na jumuiya ambazo hutekelezwa hasa na jumuiya mahalia hulinda miradi ya Wikimedia na Wanawikimedia vilevile.

Kikosi kazi cha viwango vya kawaida vya kimataifa

Ili kuunga mkono taratibu hizi muhimu za kujitawala, kikundi hiki kitauliza jinsi viwango vya kawaida zaidi vya sera za NPOV kati ya miradi ya Wikimedia vinaweza kulinda na kuboresha miradi na kusaidia wafanyakazi wa kujitolea, kwa kuhakikisha uzingatiaji makini uliotengeneza sera za NPOV katika miongo miwili iliyopita. Nia ya kikundi kazi itakuwa kuwezesha kubadilishana maarifa kuhusu sera zinazoongozwa na jumuiya ambazo zimefanya Wikipedia kuwa rasilimali inayoaminika sana duniani kote. Hii itajumuisha maoni kutoka kwa kazi inayoendelea tayari ya kuanzisha sera[3] na ambayo yanaonyesha maadili yanafuatwa na jumuiya ya kimataifa ya Wikimedia.

Mapendekezo ya awali, yanayolenga matoleo ya lugha ya Wikipedia, yatawasilishwa kwa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Wikimedia Foundation katika mkutano ujao wa Juni 2025, pamoja na uidhinishaji wa mpango na bajeti ya Shirika.

Hii inatuhitaji sote kwa pamoja

Utegemezi wa ulimwengu kwenye Wikipedia (na Wikimedia kwa ujumla) unaendelea kukua - kutoka chatbots za AI hadi injini za utafutaji hadi wasaidizi wa sauti hadi watumiaji wa maudhui kwenye mtandao. Wakati ambapo tunatumiwa (na kuhitajika!) kuliko wakati mwingine wowote, lazima tuimarishe kanuni zetu za msingi na kudumisha maadili yetu ya pamoja. Kuimarisha kutoegemea upande wowote kwa Wikipedia kutaifanya kuaminiwa zaidi kutoa maudhui ambayo mabilioni ya watu wanategemea duniani kote.

Michango inakaribishwa na wote wanaojali mada hizi ndani na nje ya harakati za Wikimedia, kwenye ukurasa huu maalum wa Meta au kama sehemu ya mazungumzo ya Mpango wa mwaka wa Shirika.

Asanteni nyote, Nat Tymkiv, Mwenyekiti wa Bodi

Maryana Iskander, Mkurugenzi mtendaji

Viungo:

Ndimi, antanana / Nataliia Tymkiv Mwenyekiti, Bodi ya Wadhamini ya Wikimedia Foundation