Mpango wa Mwaka wa Wikimedia Foundation/2023-2024/Mitindo ya Nje

From Meta, a Wikimedia project coordination wiki
This page is a translated version of the page Wikimedia Foundation Annual Plan/2023-2024/External Trends and the translation is 100% complete.

Mwaka jana, Wikimedia Foundation ilishiriki orodha ya mitindo ya nje ikichochewa na “Mafumbo na Vipaumbele” kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji Maryana Iskander katika Ziara yake ya Kusikiliza alipoingia. Mwaka huu, Shirika limeazimia kusasisha mitindo na linaomba msaada kutoka kwa harakati pana ili kushiriki mawazo yao kuhusu mada hizi. Tunapofikiria ulimwengu uliotuzunguka, mitazamo mbalimbali hutupatia picha wazi ya ukweli na maamuzi na maamuzi yenye ufahamu bora Zaidi. Tunakaribisha na kuhimiza maoni yako kuhusu rasimu ya mawazo hapa chini.

Hii ni fursa ya kutazama upande wa nje: Kama harakati, tunahitaji kuendelea kuuliza: “ulimwengu unahitaji nini kutoka kwetu sasa?” Pia ni mahali pa kuanzia kwa uelewa wa pamoja, hata kwa maoni tofauti: Uchanganuzi wa mitindo unatuhitaji kuwa mtazamo wa muda mrefu na kufuatilia kile ambacho ni muhimu kwetu - hata kama tuna maoni tofauti kuhusu jinsi ya kushughulikia.

Kwa kusema hayo, tunaishi katika ulimwengu mgumu, unaobadilika haraka. Hii si orodha pana ya vitisho na fursa zinazokabili harakati zetu, bali ni masuala machache yanayotusumbua sana.

Utafutaji & Maudhui

Sasisho kutoka 2022: majukwaa ya kijamii yanaendelea kutatiza injini za utafutaji za desturi, lakini akili bandia (AI) inatishia usumbufu mkubwa zaidi.

Matukio yanayotokana na mtu binafsi yanazidi kuwavutia watazamaji wachanga kwenye majukwaa ya kijamii (TikTok, Instagram) na mbali na injini za desturi za utafutaji. Majukwaa ya kijamii yanajaribu sifa mpya za utafutaji ili kuwashirikisha watumiaji. Injini za utafutaji za desturi zinajaribu mikakati tofauti ya kusalia na ushindani na kubaki mahali unakoenda - kitu ambacho hupunguza kiwango cha SEO cha maudhui ya Wikimedia katika viungo vya matokeo ya utafutaji wa nje.

Mlipuko wa AI ya kuzalisha ungeweza kuzalisha uundaji na utumiaji wa maarifa, lakini husababisha kutokuwa na uhukika na hatari kwa wajibu wetu katika maarifa ya mfumo wa ikolojia. Katika muda wa miezi 2 tu, ChatGPT ikawa programu ya tovuti ya watumiaji inayokua kwa kasi zaidi wakati wote. Injini za utafutaji na vivinjari vya desturi (Google, Bing, DuckDuckGo) zimeanza kufanya majaribio ya utafutaji unaosaidiwa na AI chatbot, kutumia GPT na miundo mingine mikubwa ya lugha (LLMs) - ambayo kwa kiasi fulani inategemea Wikimedia kama chanzo cha data ya mafunzo na hifadhi ya maarifa lakini si mara zote kuwakilisha au kuhusisha taarifa kutoka kwa miradi yetu kwa usahihi.

Teknolojia hizi zinaibuka na zinabadilika haraka, na zinaweza mwishowe kutumika kwa njia zinazotusaidia kuendeleza dhamira yetu - km., kwa kuongeza ufanisi katika uundaji wa maudhui, uthibiti na utiririshaji wa mchango wa kiufundi kwenye miradi yetu, pamoja na kutoa njia mpya za kufanya maudhui kupatikana na kufikika zaidi kwa msomaji. Hata hivyo, kuna vizuizi vya kuunganisha zana wasilianifu za AI katika miradi yetu - k.m., maswali wazi kuhusu hali ya hakimiliki ya zao la AI zalishi, gharama ya kudumisha na kuendesha, na wasiwasi kuhusu upendeleo na kutokuwa sahihi.

Pia kuna changamoto kubwa kwenye uendelevu wetu zilizoletwa na teknolojia hii. Matumizi ya wasaidizi wa AI kama mahali pa kuingilia kutafuta yanaweza kuzidisha changamoto zilizopo kuhusu uwasilishaji na utenganishaji, hivyo kuwatenga zaidi watumiaji kuchangia au kusaidia kifedha miradi yetu. Uundaji ulioenea wa maudhui unaosaidiwa na AI (kwenye na nje ya miradi yetu) pia huhatarisha kuendeleza miradi yetu kwa maudhui yasiyotegemewa na/au yenye madhara na kuharibu dhamira na chapa yetu bila kubatilishwa. Mnamo Machi 2023, tuliandaa mazungumzo ya kwanza kati ya yale ambayo yanaweza kuwa ya kawaida na wanajamii wanaovutiwa na mada hii ili kujadili fursa, changamoto na hatua zinazofuata.

Upotoshaji wa taarifa

Vita vya Habari vinazidi. Vita vya Habari kama silaha ya kisiasa na kijiografia ya serikali na harakati za kisiasa vinaongezeka na hali kua ngumu zaidi kuelezeka/kutambua, huku pia vikizidi kuwa hatari (kampeni za upotoshaji wa taarifa zinazidi kuambatana na vitisho vya kimwili, usaliti, kukamatwa n.k.).

Maudhui yatokanayo na machine yanapanuka. Uwezo wa mifumo bandia kutoa maudhui bora unaongezeka, na muhimu zaidi, ujumuishaji wake wa kijamii unajitokeza haraka katika masoko mengi makubwa. Jinsi Wikimedia inavyojiweka yenyewe inaweza kusaidia kuunda uwanja.

Taarifa ya uongo iliyofichwa na vekta za mashambulizi ya taarifa potofu zinaongezeka. Hofu ya faragha ya kidijitali na vita vya habari husukuma habari potofu zaidi katika njia zilizofungwa ambapo usimbaji fiche hufanya ufuatiliaji na utabiri kuwa changamoto zaidi, kuruhusu taarifa za uongo kustawi na ugawanyaji kuendelea zaidi. Kama jukwaa huria kukabiliana na mwelekeo (inafuatilika, simamiwa, kutunzwa, umma na wazi) tunaweza kuonyesha umbo/mbinu yetu kama kushughulikia tatizo kiutendaji.

Wikimedia imekuwa shabaha mashuhuri. Mnamo 2022, masimulizi ya taarifa za uongo na mashambulizi ya kujitolea dhidi ya harakati, mtu binafsi, watu wa kujitolea, na Shirika pia viliongezeka, na kusababisha hatari kubwa zaidi kwa watu wetu wa kujitolea na kwa sifa ya Shirika.

Taratibu

Wikimedia kama shirika imekuwa ya kimataifa zaidi, inayomaanisha kwamba sheria zaidi za nchi nyingi tunazizingatia. Ili kulinda miradi na watu wetu, tutahitaji kutii sheria mbalimbali zinazoongezeka duniani kote. Hii ni pamoja na sheria nchini Marekani, sheria pana katika Umoja wa Ulaya kama vile Sheria ya Huduma za Kidijitali na, kwa kila kesi, sheria katika nchi nyingine katika maeneo mbalimbali ya dunia kama vile madai ya kashfa na faragha. Ni lazima tuwe tayari kupigana dhidi ya hatua hatari za serikali mahakamani na kutetea hadharani dhidi ya sheria hatari katika nchi nyingi zaidi tunapoendelea kukua.

Zaidi inahitajika kwa watoa huduma ya uendeshaji kuliko hapo awali. Serikali ziko chini ya shinikizo kubwa la kisiasa kushughulikia mkoba wa kunyakua madhara na upendeleo mtandaoni. Mwaka huu, kesi mbili za kupinga sheria ya mtandao ya CDA 230 zitasikilizwa na Mahakama ya Juu ya Marekani, na hivyo kutatiza ulinzi wa mpatanishi ulioimarishwa vizuri ambao majukwaa kama Wikipedia hutegemea. Wakati huo huo, adhabu za kuendesha maudhui hatari zinaongezeka, ikijumuisha dhima ya uhalifu katika baadhi ya matukio kama vile Mswada wa Usalama Mtandaoni wa Uingereza.

Watunga sheria hawafikirii kuhusu Wikipedia. Sheria inaendelea kuchanganya Wikimedia na majukwaa ya faida. Watunga sera wachache wanaelewa mtindo wa kudhibiti maudhui yakujitolea wa Wikimedia. Tunahitaji kuelimisha serikali na washawishi wa sera kuhusu mtindo wa Wikimedia -- na jinsi sheria zinavyopaswa kuulinda na kuuunga mkono.

Uhusiano wetu na mifumo ya tekno ya faida ni muhimu na ngumu. Tunahitajiana. Lakini ili kulinda mtindo, miradi na watu wa Wikimedia dhidi ya udhibiti hatari, ni lazima watunga sheria na washawishi wa sera waelimishwe kuhusu jinsi tulivyo tofauti na mifumo mikubwa ya kupata faida. Ni lazima tuwekeze katika njia za kuhakikisha kuwa watunga sheria na washawishi wa sera wanaelewa jinsi mtindo wetu wa namna ya kujitolea unavyofanya kazi na nafasi nzuri ya harakati zetu katika jamii.


HistoriaMalengo