Mpango wa Mwaka wa Wikimedia Foundation/2023-2024/Historia

From Meta, a Wikimedia project coordination wiki
This page is a translated version of the page Wikimedia Foundation Annual Plan/2023-2024/History and the translation is 100% complete.

Historia ya upangaji wa Shirika

Wikimedia Foundation kwa sasa inatumia Mwelekeo wa Kimkakati wa 2017 wa “Usawa wa Maarifa na Maarifa kama Huduma” kama dira yake ya kupanga kwa miaka mingi kuelekea upeo wa mkakati wa haraki wa 2030.

Juhudi za awali kuhusu fikra za kimkakati katika Shirika ziliongozwa zaidi na watendaji wa Bodi ya Wadhamini (kwa mfano kupitia uchanganuzi wa SWOT). Mchakato wa kimkakati wa 2009-2010 ulikuwa zoezi la kwanza kutafuta maoni mengi kutoka kwa harakati. Ulilenga kuelewa na kushughulikia changamoto na fursa muhimu zinazokabili harakati za Wikimedia hadi 2015.” na “ilifikia kilele katika mfululizo wa vipaumbele na malengo, pamoja na mipango mahususi ya uendeshaji kwa Wikimedia Foundation.” Kwa kurejea nyuma, Mpango wa Kimkakati wa 2010 -2015 uliotokea sasa unakubalika kuwa ulikuwa na malengo makubwa sana, na malengo magumu kufikiwa.

Mnamo 2012, Mkurugenzi Mtendaji Sue Gardner alisema kuwa wafanyakazi wa Shirika “wamenyoshwa na kulazimishwa kupita kiasi,” na kwamba “tatizo kuu katika Wikimedia Foundation wakati huu” hakikuwa pesa, lakini badala yake “uangalifu wa shirika.” Sue alimua “ Kupunguza mwelekeo “ wa shirika, akilenga juhudi zake hasa kwenye Teknolojia na Utoaji ruzuku. Hii ilisababisha kuundwa kwa Wiki Education Foundation kama shirika tofauti lisilo la faida, ili kuanza na kupanua programu ya Elimu ya Wikimedia Foundation huko Amerika ya Kaskazini.

Mnamo 2016, Mkurugenzi Mtendaji Lila Tretikov alianzisha mjadala wa jamii kuhusu “Mkakati wa Muda” uliopendekezwa. Mchakato huu ulikuwa wa mashauriano, ukiomba maoni kuhusu mpango ulioamuliwa kabla badala ya kuundwa pamoja. Shirika lilitumia mfumo huu kuongoza mipango yake ya mwaka kwa miaka michache.

Mnamo 2017, Mkurugenzi Mtendaji Katherine Maher alizindua mchakato wa Harakati za Mkakati, juhudi kubwa ya harakati za kuamua mwelekeo wa kimkakati wa pamoja kwa upeo wa 2030. Baada ya miezi ya majadiliano, utafiti, mahojiano na matukio (Awamu ya 1), Mwelekeo wa Kimkakati uliopatikana uliidhinishwa na mashirika zaidi ya mia moja ya Wikimedia. Kati ya 2018 na 2020 (Awamu ya 2), vikundi kazi tisa vya mada vinavyojumuisha watu wa kujitolea, wafanyakazi, washirika na wadhamini walitayarisha Mapendekezo kwa ajili ya harakati ya kufanya kazi juu ya Mwelekeo. Orodha ya mwisho ya Mapendekezo (na kanuni zinazoambatana) ilichapishwa mnamo 2020.

Kati ya 2019 na 2022, shughuli za Shirika zilipangwa kulingana na Mpango wa Muda wa Kati, jaribio la kupanga miaka mingi kuongeza kazi ya Shirika hadi agizo mahususi lilipoibuka kutoka mapendekezo na utekelezaji wa Harakati za Mkakati.

Kufikia 2023, harakati sasa ziko katika Awamu ya 3 ya Harakati za Mkakati: utekelezaji kupitia Mipango iliyopewa kipaumbele. Awamu hii ya mwisho inazuiliwa haswa na uchovu wa mkakati na kukosa kasi. Ingawa Mapendekezo yanafikiriwa kuwa ya lazima, pia hayana uwezekano wa kutosha kutimiza maono ya 2030 ya harakati za Wikimedia.

Mnamo 2022, Shirika liliendelea kusisitiza mpango wake wa mwaka wa 2022-2023 katika Mwelekeo wa Kimkakati wa Harakati za Mkakati, na sasa linatafuta kufungamanisha upangaji wake wa kimkakati wa miaka mingi kwa karibu zaidi na Mwelekeo wa Harakati za Mkakati, Mapendekezo, Kanuni na miongozi mingine ya kimkakati.

Tazama pia:

  • Mkakati kwenye Meta-Wiki: Muhtasari wa juhudi zote za mkakati zinazohusiana na harakati za Wikimedia, ikiwa pamoja na viungo vya mipango ya kimkakati ya mashirika mengine ya Wikimedia.
  • Ukaguzi wa kina Zaidi wa michakato ya mkakati wa 2010–2016 uliyoandikwa kabla ya kuzinduliwa kwa mchakato wa Harakati za Mkakati za 2017.