Uchaguzi wa Wikimedia Foundation / 2021 / 2021-07-02 / 2021 Wagombea Waliothibitishwa

From Meta, a Wikimedia project coordination wiki
This page is a translated version of the page Wikimedia Foundation elections/2021/2021-07-02/2021 Confirmed Candidates and the translation is 100% complete.

Bodi ya Wadhamini ya Uchaguzi wa 2021 unafunguliwa tarehe 4 Agosti 2021. Wagombea kutoka kwenye jamii waliombwa kuwasilisha nia yao ya ugombea. Baada ya wito huu kwa wagombea uliodumu kwa wiki tatu, walipatikana wagombea 20 wa uchaguzi wa 2021.

Bodi ya Wadhamini ya Wikimedia Foundation inasimamia shughuli za Wikimedia Foundation. Bodi hii inataka kuboresha umahiri wao na utofauti kama timu. Bodi hii wametangaza maeneo ya utaalam ambayo wanatarajia kupata wadhamini wapya.

Harakati ya Wikimedia ina fursa ya kupiga kura kwa ajili ya uteuzi wa wadhamini wa jamii na washirika. Bodi hii inatarajiwa baadaye kuchagua wagombea wanne waliopigiwa kura zaidi kuwa wadhamini, kuanzia Septemba, kwa kipindi cha miaka mitatu.

Je unawezaje kushiriki?

Jifunze zaidi kuhusu wagombea

Wagombea kutoka harakati zote wamewasilisha wagombea wao. Jifunze juu ya kila mgombea kuitendea haki kura yako. Jumuiya iliwasilisha maswali kwa wagombea kujibu wakati wa kampeni. Wagombea watajibu orodha ya maswali ya jamii yaliyokusanywa na kamati ya uchaguzi ya Meta. Katika wiki zijazo, wagombea watapata fursa ya kuwasilisha video zao wakizungumza juu ya ugombea wao. Shiriki katika shughuli za kampeni

Shiriki katika shughuli za kampeni

Timu ya wawezeshaji wanaounga mkono uchaguzi huu wa Bodi imepanga kufanya shughuli kadhaa kwa kipindi cha kampeni. Shughuli hizi zinaweza kupatikana kwenye ukurasa Meta wa uchaguzi wa Bodi.

Wanajamii wanahimizwa kupanga shughuli katika jamii zao. Tunauliza kwamba shughuli zozote zinazokusudiwa kuwashirikisha wagombea zibaki zinaheshimu wakati wao, kwani kugombea kunaweza kuchukua muda mwingi. Tafadhali orodhesha shughuli unazopanga kwenye ukurasa wa Meta wa uchaguzi wa Bodi ili watu zaidi waweze kuzipata. Wawezeshaji na wanaojitolea kwa ajili ya uchaguzi wanapatikana ikiwa unahitaji msaada.

Piga kura

Upigaji kura kwa ajili ya uchaguzi wa Bodi ya Wadhamini ya 2021 unafunguliwa tarehe 4 Agosti 2021 na kufungwa tarehe 17 Agosti 2021. Kamati ya Uchaguzi ilichagua Kura Moja inayoweza kuhamishwa kuwa mfumo wa upigaji kura. Pata maelezo zaidi kuhusu mahitaji ya upigaji kura, mchakato, na maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu upigaji kura.

Kura Moja inayoweza kuhamishwa

Mfumo huu wa upigaji kura unawaruhusu wapiga kura kuorodhesha wagombea kwa upendeleo. Hii inasaidia wapiga kura kushiriki matakwa yao wazi zaidi kuliko kukubali kirahisi au kupinga kura. Ikiwa mgombea wako wa uchaguzi mkuu tayari ana kura za kutosha za kuchaguliwa au hatashinda, kura yako itahamishiwa kwa mgombea wako wa chaguo la pili. Nakadhalika. Timu ya uwezeshaji ilikuja na mfano wa kufurahisha. Habari zaidi itakuja katikati ya Julai.

Tafadhali sambaza ujumbe ili watu wengi waweze kusaidia kupata wagombea bora kusaidia kuongoza Wikimedia Foundation na kuunga mkono mahitaji ya harakati kwa miaka michache ijayo.

Katika ubora,

Kamati ya Uchaguzi