Mwongozo wa Kimataifa wa Mwenendo na Maadili/Kamati ya Uratibu/Katiba/Taarifa za Mpiga Kura

From Meta, a Wikimedia project coordination wiki
This page is a translated version of the page Universal Code of Conduct/Coordinating Committee/Charter/Voter information and the translation is 96% complete.
Outdated translations are marked like this.

VOTE HERE

Universal Code of Conduct

Kura ya "kuidhinisha katiba ya Kamati ya Kuratibu ya Mwongozo wa Kimataifa wa Mwenendo na Maadili" (U4C) itafunguliwa kuanzia tarehe 19 Januari hadi 2 Februari 2024 23:59:59 (UTC) kwa njia ya Secure Poll. Wapigakura wote wenye sifa ya kupiga kura ndani ya jumuiya ya Wikimedia wana fursa ya kuunga mkono au kupinga kupitishwa kwa Katiba ya U4C, na kusema kwa nini wanapinga. Kuidhinishwa kwa katiba ni muhimu ili kuweka kanuni na taratibu za kamati hii mpya. Taarifa zaidi kuhusu madhumuni na upeo wa U4C zinaweza kupatikana hapa. Pata maelezo zaidi kuhusu maelekezo ya kupiga kura na ustahiki wa mpiga kura hapa chini.

Tafadhali pitia Maswali yaulizwayo mara kwa mara kuhusu upigaji kura kwa maelezo zaidi kuhusu kupiga kura.

Mchakato wa Upigajikura

Ikiwa unastahiki kupiga kura:

  1. Kagua Katiba ya U4C.
  2. Amua ikiwa utaunga mkono au kupinga kupitishwa kwa Katiba hiyo. Ikiwa unapinga, andika mabadiliko unayopendekeza yafanyike kwenye Katiba hiyo ili kujumuisha pamoja na kura yako.
  3. Jifunze jinsi ya kurekodi kura yako kwenye SecurePoll.
  4. Nenda kwenye ukurasa wa kupigia kura wa SecurePoll na ufuate maelekezo.
  5. Wakumbushe wanajamii wengine kupiga kura!

Nini kinapigiwa kura?

Mojawapo ya mapendekezo muhimu ya malengo ya kimkakati ya 2030 ilikuwa uundaji shirikishi wa UCoC na miongozo ya utekelezaji ili kutoa msingi wa kimataifa wa tabia inayokubalika kwa harakati nzima bila kuvumilia unyanyasaji.

Miongozo ya Utekelezaji (EG) ya UCoC iliidhinishwa na Wanawikimedia mnamo Januari 2023, na kuidhinishwa na Baraza la Wadhamini mnamo Machi 2023. EG inataka kuundwa kwa kamati ya kuratibu matumizi ya UCoC katika miradi yote ya Wikimedia. Ili kufanya kazi vizuri na kufanya kazi na vikundi na michakato ya jumuiya iliyopo, Katiba ya kamati hii mpya inahitajika. Katiba iliandikwa na U4C Kamati ya Uundaji ya Kujitolea.


Ni nini kimo kwenye Katiba ya U4C?

Kutoka kwenye muhtasari wa Katiba:

Hati ya rasimu ya Kamati ya Kuratibu ya Kanuni za Maadili ya Jumla (U4C) inaelezea sera, taratibu na michakato ambayo itaongoza kazi ya U4C.

Sehemu za awali za rasimu hiyo zinaelezea mpangilio wa Kamati, ikijumuisha madhumuni na upeo wa kazi ya Kamati, majukumu yake na kustahiki na michakato ya uchaguzi kwa wajumbe wa Kamati.

Vifungu vifuatavyo vinashughulikia matarajio ya ndani kuhusu mwenendo, kujiondoa na uwazi na usiri wa kazi ya Kamati. Sehemu zilizosalia zinashughulikia michakato ya kufuatilia, kukagua na kuunga mkono UCoC na Miongozo ya Utekelezaji. Pia inashughulikia utoaji wa zana na mafunzo kwa jamii kutumia pamoja na UCoC na Miongozo ya Utekelezaji na vile vile jinsi U4C itakavyohusika na kuingiliana na Shirka la Wikimedia Foundation na miundo mingine ya kiutawala ya harakati.

Katiba hii ilikaguliwa na jumuiya za Wikimedia mnamo Septemba 2023, na masahihisho yakafanywa kulingana na maoni ya jumuiya.

Kwanini upige kura?

Ni muhimu kwamba U4C ifanye kazi vyema na miundo iliyopo ya utawala wa jumuiya na kuakisi maadili ya jumuiya. Katiba thabiti itasaidia Kamati kufuatilia jinsi UCoC inavyotumika katika jumuiya zetu, na kuipa zana inayohitaji kutatua matatizo ya utekelezaji yanapotokea.

Jinsi ya kupiga kura

Muhtasari wa kura ya SecurePoll. Kumbuka hususani kwamba votewiki inaweza kuonesha kuwa hujaingia. Kura yako bado itahesabiwa.

Tafadhali soma sehemu hii kabla ya kwenda kwenye SecurePoll ili kujifunza taarifa muhimu ili kufanya uzoefu wako wa kupiga kura uende vizuri.

Sehemu ya kupigia kura itatoa swali la kupiga kura, na kukupa machaguo mawili: "Hapana" na "Ndiyo"

  • Kisanduku cha "Maoni" kitakupa mahali pa wewe kuacha maoni yako kuhusu masuala yoyote uliyo nayo na miongozo inayopendekezwa.
  • Kisha SecurePoll itakujulisha kuwa kura yako imerekodiwa.
  • Unaweza kurudia kupiga kura tena katika uchaguzi. Kura yako ya awali itabatilishwa . Unaweza kufanya hivyo mara nyingi unavyopenda.

Je, matokeo ya upigaji kura yataamuliwaje?

Kiwango cha juu cha usaidizi cha zaidi ya 50% cha watumiaji wanaoshiriki kitahitajika ili kuendelea na uchaguzi wa Kamati mpya. Kwa sasa, vuguvugu hili halina mtindo mmoja kuhusu kupita/kushindwa kwa michakato ya upigaji kura ya kufuata (baadhi ya michakato hutumia dhana karibu na walio wengi zaidi (⅔), huku wengine wakitumia mtindo rahisi wa uwingi (50% +1), huku wengine wakiepuka kura ya kuhesabu kabisa). Kwa mchakato huu, ili kuuweka sambamba na kura nyingi za maoni katika mamlaka ya ulimwengu halisi, kura rahisi ya wengi ilichaguliwa.

Wapiga kura wataulizwa ni vipengele vipi vinahitaji kubadilishwa na kwa nini. Iwapo kura itazalisha kura nyingi za "hapana", timu ya mradi wa UCoC itaficha jina na kuchapisha sababu zilizotolewa na wapiga kura wa "hapana". Wajumbe wa Kamati ya Ujenzi ya U4C wataangalia uboreshaji wa Katiba kulingana na hoja zilizotolewa katika mchakato wa kupiga kura. Sawa na mchakato huu, masahihisho yatachapishwa kwa ukaguzi, na kura ya pili itafanyika.

Je, watu walio nje ya Shirika la Wikimedia Foundation watahusishwa katika kuchunguza kura ili kuthibitisha uhalisia?

Matokeo ya kura yatachunguzwa kwa dosari na watu Wanawikimedia wasio wafanyakazi walio na uzoefu katika upigaji kura wa harakati na michakato ya uthibitishaji. Wachunguzi wa kura ni:

Ustahiki wa kupiga kura

Ustahiki wa kupiga kura umewekwa na Bodi ya Wadhamini ya Wikimedia. Wachangiaji wote waliosajiliwa wa Wikimedia ambao wanakidhi mahitaji ya msingi zaidi ya shughuli, wafanyakazi na wakandarasi washirika na Shirika la Wikimedia Foundation (walioajiriwa kabla ya tarehe 28 Novemba 2023), na wadhamini wa sasa na wa zamani wa Shirika la Wikimedia Foundation, watapata fursa ya kupigia kura Katiba inayopendekezwa katika SecurePoll.

Wahariri

Unaweza kupiga kura kwa kutumia akaunti yoyote iliyosajiliwa unayomiliki kwenye Wikimedia wiki. Unaweza kupiga kura mara moja pekee, bila kujali unamiliki akaunti ngapi. Ili kukidhi vigezo, akaunti hii moja lazima:

  • isiwe imezuiliwa katika zaidi ya mradi mmoja;
  • na isiwe bot;
  • na iwe imefanya angalau mabadiliko 300 kabla ya tarehe 28 Novemba 2023 kwenye Wikimedia;
  • na imefanya angalau mabadiliko 20 kati ya 16 Juni 2023 na 16 Desemba 2023.

Zana ya Kuhakikisha Ustahiki wa Akaunti inaweza kutumika kuthibitisha kwa haraka ustahiki msingi wa kupiga kura wa mhariri.

Wasanidi

Wasanidi programu wana sifa za kupiga kura ikiwa:

  • ni wasimamizi wa seva za Wikimedia walio na ufikiaji wa nje
  • au wameweka angalau ahadi moja iliyounganishwa kwa Wikimedia repos kwenye Gerrit, kati ya 16 Juni 2023 na 16 Desemba

Vigezo vya ziada:

  • au umeweka angalau ahadi moja iliyounganishwa kwenye repo yoyote katika nonwmf-extensions au nonwmf-skins, kati ya 16 Juni 2023 na 16 Desemba
  • au umeweka angalau ahadi moja iliyounganishwa kwenye repo yoyote ya zana ya Wikimedia (kwa mfano magnustools) kati ya tarehe 16 Juni 2023 na 16 Desemba.
  • au umefanya angalau mabadiliko 300 kabla ya tarehe 16 Desemba 2023 na umefanya angalau mabadiliko 20 kati ya tarehe 16 Juni 2023 na 16 Desemba kwenye translatewiki.net.
  • au mmoja wa watunzaji/wachangiaji wa zana zozote, roboti, hati za watumiaji, vifaa na moduli za Lua kwenye kwenye tovuti za wiki za Wikimedia.
  • au umejihusisha kwa kiasi kikubwa katika kubuni na/au kukagua michakato ya maendeleo ya kiufundi inayohusiana na Wikimedia.

Kumbuka: Ikiwa unakidhi vigezo vikuu, utaweza kupiga kura mara moja. Kwa sababu ya vikwazo vya kiufundi vya SecurePoll, watu wanaokidhi vigezo vya ziada huenda wasiweze kupiga kura moja kwa moja, isipokuwa wakitimiza vigezo vingine. Iwapo unafikiri unakidhi vigezo vya ziada, tafadhali tuma barua pepe ucocproject@wikimedia.org ukiwa na sababu angalau siku nne kabla ya tarehe ya mwisho ya kupiga kura.

Wafanyakazi na wakandarasi wa Wikimedia Foundation

Wafanyakazi wa sasa wa Wikimedia Foundation na wafanyakazi wasio wa kudumu wanaweza kupiga kura ikiwa wameajiriwa na Shirika la Wikimedia Foundation kuanzia tarehe 28 Novemba 2023.

Wafanyakazi na wakandarasi wa washirika wa Wikimedia

Chapta za sasa za Wikimedia, Shirika la Kimada au wafanyakazi wa kikundi cha watumiaji na wanaajiriwa wasio wa kudumu wana sifa za kupiga kura ikiwa wameajiriwa na shirika lao kuanzia tarehe 28 Novemba 2023.

Wajumbe wa bodi ya Wikimedia Foundation

Wanachama wa sasa na wa zamani wa Bodi ya Wadhamini ya Wikimedia Foundation wana sifa za kupiga kura.

Maswali ya mara kwa mara kuhusu Upigaji kura

  1. Ninawezaje kuthibitisha kustahiki kwangu? Wahariri wanaweza kutumia zana ya Kuhakiki ustahiki wa Akaunti ili kuthibitisha kuwa unakidhi vigezo katika uchaguzi wa sasa. Ukurasa wa taarifa za michango kwenye miradi yote ya wiki unapatikana ili kupata maelezo zaidi kuhusu idadi ya mabadiliko na historia ya michango.
  2. Masharti ya kujiunga yanawekwaje? Haya ni masharti yale yale yanayotumika kwa uchaguzi wa Baraza la Wadhamini.
  3. Mpiga kura unayestahiki ikiwa huwezi kupiga kura unaweza kupokea ujumbe: "Samahani, haumo katika orodha iliyoamuliwa hapo awali ya watumiaji walioidhinishwa kupiga kura katika uchaguzi huu." Hakikisha kuwa umeingia. Hakikisha unapiga kura kwenye Meta-wiki, unaweza kutumia kiungo hiki kwenda kwenye ukurasa wa kuanza kupiga kura. Ikiwa wewe ni msanidi programu, mfanyakazi wa Wikimedia Foundation au mwanachama wa Bodi ya Ushauri, huenda hatukuweza kukulinganisha na jina mahususi la mtumiaji. Unapaswa kuwasiliana na ucocproject@wikimedia.org ili kuongezwa kwenye orodha. Iwapo bado huwezi kupiga kura na unaamini una sifa za kupiga kura unaweza kuacha ujumbe kwenye ukurasa wa mazungumzo ya uchaguzi au wasiliana na ucocproject@wikimedia.org. Jibu linapaswa kutumwa ndani ya masaa 72.
  4. Siwezi kuingia katika VoteWiki. Huhitaji kuingia katika VoteWiki ili kupiga kura. Ukiona tu dodoso la kupigia kura, basi ujue SecurePoll imefanikiwa kukutambua. Kwa sababu za usalama, ni idadi ndogo tu ya akaunti zimesajiliwa kwenye VoteWiki.
  5. Kuna mtu anayeweza kuona jinsi nilivyopiga kura? Hapana, uchaguzi uko salama. Uchaguzi unatumia programu ya SecurePoll. Kura ni siri. Hakuna yeyote kutoka kwa Bodi au mtu yeyote kwenye wafanyakazi wa Shirika la Wikimedia Foundation anayeweza kuzifikia. Mwanachama wa timu ya Trust & Safety katika Shirika la Wikimedia Foundation ana ufunguo wa usimbaji fiche kwa ajili ya uchaguzi. Mara ufunguo ukiwashwa, uchaguzi unasimamishwa.
  6. Ni data gani inayokusanywa kuhusu wapigakura? Baadhi ya data zinazoweza kuwatambulisha wapigakura zinaweza kuonekana na watu wachache waliochaguliwa ambao hukagua na kujumlisha matokeo. Tazama wakaguzi wa uidhinishaji kama ilivyotangazwa hapo juu. Hii inajumuisha anwani ya IP na wakala wa mtumiaji. Data hii hufutwa kiotomatiki siku 90 baada ya uchaguzi.
  7. Data hii itatumika vipi? Vipimo kuhusu uchaguzi huu vitafupishwa kwenye matokeo ya kurasa za uchaguzi kwenye Meta na ripoti ya baada ya uchambuzi wa uchaguzi. Hakuna maelezo ya kibinafsi yatakayochapishwa. Maelezo haya yanayoweza kumtambulisha mtu binafsi yanaweza kutumiwa kubainisha idadi ya wapigakura huru na kuenea kwa wapiga kura duniani kote.
  8. Ninapopiga kura, sioni mrejesho kwamba kura ilipokelewa, na ujumbe wa kiotomatiki unaonekana ukisema kwamba nahitaji kuingia ili kupiga kura. Nini kinaendelea? Huhitaji kuingia kwenye votewiki ili kupiga kura. Hitilafu hii inawezekana ni suala la kuhifadhi. Tunaomba radhi kwa usumbufu huu: tafadhali jaribu kupiga kura tena katika ukurasa wa kuoigia kura wa SecurePoll. Hii inapaswa kukuarifu kwa ujumbe unaosema "Kura itapigwa kwenye wiki kuu. Tafadhali bofya kitufe kilicho hapa chini ili kupelekwa huko." Kubofya kitufe kutakupeleka kwenye seva ya kupiga kura na kunapaswa kukuruhusu kupiga kura. Pia kumbuka kuwa uko huru kukabidhi au kubadilisha mapendeleo yako ya kupiga kura mara nyingi upendavyo. Kura moja pekee kwa kila mtumiaji itahifadhiwa, na mfumo utabadilisha kura zako za zamani na kuweka mpya, na kufuta kura zozote za awali. Mchakato wako wa kupiga kura unapokamilika, risiti itaonyeshwa kwenye skrini yako, ambayo unaweza kuhifadhi kama ushahidi kwamba umepiga kura.
  9. Mfumo wa upigaji kura unalindwa vipi dhidi ya watumiaji kuingiza kura nyingi? Kura moja pekee kwa kila mtumiaji huhifadhiwa kwenye mfumo. Uko huru kukabidhi au kubadilisha mapendeleo yako ya kupiga kura mara nyingi upendavyo. Mfumo huu utachukua nafasi ya kura zako za zamani na kuweka mpya, na kufuta kura zozote za awali.
  10. Je, wafanyakazi wanalazimishwa au wanahimizwa kupiga kura kwa njia mahususi? Hapana, wafanyakazi wa Shirika la Wikimedia Foundation na wale wa washirika hawahimizwi kupiga kura kwa njia maalum. Tunahimiza kila mtu kupiga kura kwa uhuru. Ili Katiba ifanye kazi, tunahitaji maoni ya uaminifu ili kutusaidia kutambua ikiwa kuna maeneo ya uboreshaji unaohitajika.
  11. Je, Timu ya Uaminifu na Usalama ina upendeleo kuhusiana na matokeo ya kura? Kitengo cha Uaminifu na Usalama kina mihimili mitatu: Sera, Upotoshaji, na Utendajikazi. Timu inayosimamia UCoC ni timu ya Sera. Timu ya Sera haihusiki katika uchunguzi wa tabia ya mtumiaji. Ingawa haiaminiki kuwa timu ya Operesheni ina upendeleo au itakuwa na upendeleo, utenganishaji huu wa majukumu ulifanywa kimakusudi ili kuepuka upendeleo usiotarajiwa. Timu ya Sera haitathminiwi ikiwa hati hii iliyoundwa kwa ushirikiano inafikia kibali wakati wa utekelezaji wake wa kwanza au maendeleo zaidi yanahitajika. Timu hata hivyo inatathminiwa ikiwa inafanya kazi vyema na jamii. Hii inamaanisha kukuza mbinu shirikishi ya kutekeleza UCoC ambayo itafanya kazi kwenye jamii. Lengo letu ni kutimiza wajibu huo vizuri iwezekanavyo.
  12. Maswali mengine ambayo hayajatajwa hapa Kwa hitilafu za kiufundi au za mfumo wa kura, tafadhali tuma barua pepe kwenda ucocproject@wikimedia.org. Tafadhali andika jina la mtumiaji unalojaribu kupiga kura nalo na mradi ambao unajaribu kupiga kura. Mwanachama wa timu ya mradi atajibu barua pepe yako haraka iwezekanavyo.