Chaguzi za Wikimedia Foundation/2022/Upigaji Kura wa Jumuiya

From Meta, a Wikimedia project coordination wiki
This page is a translated version of the page Wikimedia Foundation elections/2022/Community Voting and the translation is 83% complete.
Outdated translations are marked like this.

Uchaguzi wa Bodi ya Wadhamini wa 2022 utakuwa kuanzia tarehe 23 Agosti 2022 hadi tarehe 6 Septemba 2022.

Wanachama wa jumuiya ya Wikimedia wana fursa ya kuwachagua wagombea wawili kwa muhula wa miaka mitatu. Ukurasa huu una maagizo ya kupiga kura. Wanajamii wanasoma miongozo ya ustahiki wa mpiga kura na Maswali yaulizwayo mara kwa mara.

Piga kura

Ikiwa unastahiki kupiga kura:

  1. Soma matamko ya Mgombea na uone ukadiriaji wa Kamati ya Uchambuzi wa kila mgombea
  2. Soma majibu ya majibu ya watahiniwa kwa maswali yaliyoulizwa na Wawakilishi wa Washirika
  3. Watch the videos recorded by the candidates answering 6 questions from the community; there is also a text version, including additional questions from the community.
  4. Tumia Dira ya Uchaguzi ili kukusaidia kuongoza uamuzi wako wa kupiga kura (based on answers to 15 additional community-sourced questions).
  5. Amua ni wagombea gani utawaunga mkono.
  6. Nenda kwenye ukurasa wa kupigia kura wa SecurePoll.
  7. Fuata maelekezo kwenye ukurasa huo.

Jinsi ya kupiga kura

Mfano wa muonekano wa sehemu ya kupigia kura ya SecurePoll kama ambavyo wapiga kura wataona.

Chini ni taarifa muhimu ili kuhakikisha matumizi yako ya kupiga kura yanakwenda vizuri. Tafadhali soma sehemu hii kwa makini kabla ya kwenda kupiga kura.

  • Uchaguzi huu unatumia muundo wa Kura Moja inayoweza Kuhamishwa. Maelezo ya mchakato wa kukokotoa yanaweza kupatikana hapa.
  • Katika ukurasa wa kupigia kura, mpiga kura ataona mlolongo wa visanduku kunjuzi. Mpiga kura atawapangilia wagombea kwa nafasi kutokea "Pendeleo 1" (anayependekezwa zaidi) hadi "Pendeleo la 6" (anayependekezwa kidogo).
  • Kuanzia juu, mpiga kura ataanza kuorodhesha wagombea anaoona wanafaa zaidi kuchaguliwa. Wagombea ambao mpiga kura anaamini kuwa hawafai kabisa wanapaswa kutiwa alama kwenye sehemu ya chini ya orodha yao.
  • Mpiga kura anaweza kuacha kuorodhesha wagombea wakati wowote wakati wa mchakato wa kupiga kura. Kwa mfano, kati ya wagombea 6, mpiga kura anaweza tu kuorodhesha 4 bora na kuwaacha wa 2 waliosalia.
  • Wagombea wanahitaji kuorodheshwa bila kuruka nambari katikati. Kuruka nambari kutasababisha hitilafu.
  • Mpiga kura hatakiwi kuorodhesha mgombea yule yule mara nyingi. Kuorodhesha mgombea yule yule mara nyingi kutasababisha hitilafu.
  • Watu wanaweza kupiga kura tena katika uchaguzi. Inabatilisha kura yao ya awali. Wanaweza kufanya hivi mara nyingi wapendavyo.